Mwimbieni, mwimbieni kwa zaburi; Zitafakarini ajabu zake zote.
Mwimbieni Bwana zaburi, Enyi watauwa wake. Na kufanya shukrani. Kwa kumbukumbu la utakatifu wake.
Pazeni zaburi, pigeni matari, Kinubi chenye sauti nzuri, na kinanda.
Tuje mbele zake kwa shukrani, Tumfanyie shangwe kwa zaburi.
Mshangilieni Bwana, nchi yote, Inueni sauti, imbeni kwa furaha, imbeni zaburi.
Mwimbieni Bwana zaburi kwa kinubi, Kwa kinubi na sauti ya zaburi.
Rehema na hukumu nitaziimba, Ee Bwana, nitakuimbia zaburi.
Mwimbieni, mwimbieni kwa zaburi, Zitafakarini ajabu zake zote.
Ee Mungu, moyo wangu u thabiti, Nitaimba, nitaimba zaburi, Naam, kwa utukufu wangu.
Ee Bwana, nitakushukuru kati ya watu, Nitakuimbia zaburi kati ya mataifa.
Nitakushukuru kwa moyo wangu wote, Mbele ya miungu nitakuimbia zaburi.
Maana, Daudi mwenyewe asema katika chuo cha Zaburi, Bwana alimwambia Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume,
Kisha akawaambia, Hayo ndiyo maneno yangu niliyowaambia nilipokuwa nikali pamoja nanyi, ya kwamba ni lazima yatimizwe yote niliyoandikiwa katika Torati ya Musa, na katika Manabii na Zaburi.
Kwa maana imeandikwa katika chuo cha Zaburi, Kikao chake na kiwe ukiwa, Wala asiwepo mtu mwenye kukaa humo;
ya kwamba Mungu amewatimizia watoto wetu ahadi hiyo, kwa kumfufua Yesu; kama ilivyoandikwa katika Zaburi ya pili, Wewe ndiwe Mwanangu, mimi leo nimekuzaa.
Basi, ndugu, imekuwaje? Mkutanapo pamoja, kila mmoja ana zaburi, ana fundisho, ana ufunuo, ana lugha, ana tafsiri. Mambo yote na yatendeke kwa kusudi la kujenga.
Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu.