Nahori akaishi miaka ishirini na kenda, akamzaa Tera.
Nahori akaishi baada ya kumzaa Tera miaka mia na kumi na kenda, akazaa wana, waume na wake.
Tera akaishi miaka sabini, akamzaa Abramu, na Nahori, na Harani.
Na hivi ndivyo vizazi vya Tera. Tera akamzaa Abramu, na Nahori, na Harani. Harani akamzaa Lutu.
Harani akafa kabla ya baba yake Tera katika nchi aliyozaliwa, yaani, katika Uru wa Wakaldayo.
Tera akamtwaa Abramu mwanawe, na Lutu mwana wa Harani, mwana wa mwanawe, na Sarai mkwewe, mke wa Abramu mwanawe, wakatoka wote katika Uru wa Wakaldayo, waende nchi ya Kanaani, wakafika mpaka Harani wakakaa huko.
Siku za Tera zilikuwa miaka mia mbili na mitano; Tera akafa katika Harani.
Wakasafiri kutoka Tahathi wakapanga Tera.
Wakasafiri kutoka Tera, wakapanga Mithka.
na Serugi, na Nahori, na Tera;